Nyimbo Za Kristo | Song Logic

NZK 118 – Nilipotoka Kabisa

118. Nilipotoka Kabisa

I've Wandered Far Away From Home (SDAH 296)

Key: A♭ Major

1

Nilipotoka kabisa, sasa narudi;
Nikakawia dhambini, Bwana narudi.

Narudi nyumbani: daima kwako.
Kwa upendo nipokee: Naja nyumbani.

2

Nikasusurika sana, sasa narudi;
Mwenye uchungu natubu, Bwana narudi.

Narudi nyumbani: daima kwako.
Kwa upendo nipokee: Naja nyumbani.

3

Nimechoka maovuni, sasa narudi;
Pendo lako lanivuta, Bwana narudi.

Narudi nyumbani: daima kwako.
Kwa upendo nipokee: Naja nyumbani.

4

Ndilo tumaini langu, sasa narudi;
Yesu alinifilia, Bwana narudi.

Narudi nyumbani: daima kwako.
Kwa upendo nipokee: Naja nyumbani.

5

Damu yake yanitosha, sasa narudi;
Unioshe kenyekenye, Bwana narudi.

Narudi nyumbani: daima kwako.
Kwa upendo nipokee: Naja nyumbani.