52. Nipe Biblia
Give Me the Bible (SDAH 272)
Key: G Major
Nipe Biblia nyota ya furaha, wapate nuru wasafirio;
Hakuna la kuzuia amani, Kwani Yesu alituokoa.
Nipe Biblia neno takatifu, Nuru yako itaniongoza,
Sheria na ahadi na upendo, Hata mwisho vitaendelea.
Nipe Biblia nihuzunikapo ikinijaza moyoni dhambi ;
Nipe neno zuri la Bwana Yesu, Nimwone Yesu Mwokozi wangu.
Nipe Biblia neno takatifu, Nuru yako itaniongoza,
Sheria na ahadi na upendo, Hata mwisho vitaendelea.
Nipe Biblia nipate kuona, hatari zilizo duniani;
Nuru ya neno lake Bwana Yesu, Itaangaza njia ya kweli.
Nipe Biblia neno takatifu, Nuru yako itaniongoza,
Sheria na ahadi na upendo, Hata mwisho vitaendelea.
Nipe Biblia taaa ya maisha; Mfariji tunapofiliwa;
Unionyeshe taa ya mbinguni, Nione utukufu wa Bwana
Nipe Biblia neno takatifu, Nuru yako itaniongoza,
Sheria na ahadi na upendo, Hata mwisho vitaendelea.