22. Usinipite, Mwokozi
Pass Me Not, O Gentle Savior (SDAH 569)
Key: G Major
1
Usinipite , Mwokozi, unisikie;
Unapozuru wengine, usinipite.
Bwana, Bwana, unisikie;
Unapozuru wengine, usinipite.
2
Kiti chako cha rehema, nakitazama;
Magoti napiga pale, nisamehewe.
Bwana, Bwana, unisikie;
Unapozuru wengine, usinipite.
3
Sina ya kutegemea, ila wewe tu;
Uso wako uwe kwangu, nakuabudu.
Bwana, Bwana, unisikie;
Unapozuru wengine, usinipite.
4
Wewe tu u mfariji: sina mbinguni,
Wala duniani pote, Bwana mwingine.
Bwana, Bwana, unisikie;
Unapozuru wengine, usinipite.